Monday 20 June 2016

'MASTER PLAN' YA JIJI LA ARUSHA KUKAMILIKA AGOSTI MWAKA HUU

Arusha 
ZIARA ya Rais Msataafu Jakaya Kikwete aliyoifanya nchini Singapole wakati wa utawala wake imeanza kuzaa matunda katika Jiji la Arusha baada ya Mpango kabambe (Master Plan) ya Jiji la Arusha kukamilika.

Mmoja wa washiriki wa mkutano wa kujadili rasimu ya tano na sita ya mpango kabambe wa jiji la Arusha (Master Plan), Godwin Abeid akisikiliza mada kwa makini
Hayo yalielezwa jijini hapa jana kwenye mkutano wa mwisho wa uwasilishaji rasimu ya utekelezaji wa mpango kabambe kwa wadau wa maendeleo wa Halmashauri ya jiji la Arusha na viunga vyake.


Akizungumza mjini hapa Mkurugenzi Msaidizi Mpango Kabambe kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Mkazi Amulike Mahenge alisema, mpango huo umelenga katika kuboresha majiji mawili ambayo ni Mwanza kwa eneo la Nyamagana na Jiji la Arusha.
Washiriki wa Mkutano wa kujadili rasimu ya mpango kabambe wa Jiji la Arusha wakimsikiliza mtoa mada (hayupo pichani), katika ukumbi wa mikutano hoteli ya Lush Garden jijini Arusha

No comments:

Post a Comment