Friday, 8 February 2013

PICHA MBALIMBALI WANACHAMA WA APC WAKIWA KWENYE MKUTANO WA MABADILIKO YA KATIBA YA APC, MKUTANO HUO ULIFANYIKA UKUMBI WA MAKUMBUSHO JIJINI ARUSHA TAR2/2/013










SIKU MKURUGENZI MTENDAJI WA UTPC ALIPOTEMBELEA OFISI ZA APC

kutoka kushoto Martin Taylor mkurugenzi wa shirika la Good Earth Trust Tanzania, Abubakar Karsan Mkurugenzi Mtendaji wa umoja wa klabu za waandishi wa habari TANZANIA (UTPC), Claud Gwandu (Mwenyekiti wa APC), na Eliya Mbonea (Katibu Mkuu wa APC),

Mkurugenzi wa UTPC Abubakar Karsani akizungumza na Mwenyekiti wa APC Claud Gwandu (katikati), na anayeshuhudia ni Mkurugenzi wa Good Earth Trust Martin Taylor walipotembelea ofisi za APC, ambapo Karsani aliukabidhi uongozi wa APC Kamera ya kisasa ya video, ikiwa ni sehemu ya mradi wa kuboresha ofisi za press clubs.

Mkurugenzi wa UTPC Abubakar Karsan (katikati), akitoa maelezo kwa viongozi wa juu wa APC, Claud Gwandu (MWENYEKITI ), Kushoto na Eliya Mbonea(Katibu Mkuu wa APC).

Thursday, 7 February 2013

MAGUNIA MENGINE 97 YA BANGI YAKAMATWA NA JESHI LA POLISI ARUSHA

Askari wa jeshi la polisi wakiwa wanashusha magunia ya madawa ya kulevya aina ya bangi mara baada ya kukamatwa eneo la Usa River wilayani Arumeru yakiwa yanasafirishwa kwenye gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T.282 AAJ kuelekea Moshi (Picha na Rashid Nchimbi wa jeshi la Polisi Arusha)

Na Mwandishi Maalum, Arusha
Jeshi la Polisi mkoani hapa limemkamata mtu mmoja akiwa na magunia 97 ya madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikuwa yanasafirishwa toka mkoani hapa kuelekea Moshi. Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas amesema.

kwamba, tukio hilo lilitokea muda wa saa 10:00 alfajiri eneo la Usa River wilayani Arumeru.
Alisema mafanikio hayo yametokana na ushirikiano mzuri kati ya jeshi hilo na wananchi ambapo taarifa za tukio hilo zilitolewa na raia wema ambapo askari wa jeshi hilo waliweka mtego eneo hilo na kufanikiwa kulikamata gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T. 282 AAJ.

Kamanda Sabas aliongeza kwa kusema kwamba, ndani ya bodi ya gari hilo kulikuwa na mboga aina ya kabeji iliyosambazwa vizuri huku chini ya mboga hiyo kukiwa na madawa hayo yaliyokuwa kwenye magunia huku yakivingirishwa kwenye mifuko ya “plastiki” kwa ndani.

Alisema katika gari hilo kulikuwa na watu watatu na mara baada ya askari hao kulisimamisha dereva pamoja na msaidizi wake walifanikiwa kukimbia huku mtu mmoja aliyejulikana kwa jina la Praygod Marick (22) Mkazi wa Dar esalaam akikamatwa.

Jeshi la polisi Mkoani hapa linaendelea kumhoji mtuhumiwa huyo huku watuhumiwa wengine wakiendelea kutafutwa. Kwa mara nyingine tena Kamanda huyo aliendelea kuwashukuru wananchi wa Mkoa huu kutokana na ushirikiano wao mkubwa wanaoutoa kwa jeshi hilo na kuendelea kuwasisitizia kuimarisha mahusiano na jeshi hilo.

Kwa muda wa kipindi cha mwezi mmoja toka januari 07, 2013 mpaka hivi leo jeshi hilo limeshakamata madawa ya kulevya aina ya mirungi magunia 372 katika magari mawili tofauti na pia limeshakamata jumla ya magunia 117 ya madawa ya kulevya aina ya bangi ambapo mwanzoni mwa wiki hii jumla ya magunia 20 yalikamatwa yakiwa yanasafirishwa kwa kutumia wanyama aina ya Punda maeneo ya Losoiti wilayani Longido.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi Liberatus Sabas akiwaonyesha waandishi wa habari madawa ya kulevya aina ya bangi ambayo yalikuwa kwenye magunia 97 yaliyokamatwa na askari wa jeshi hilo katika eneo la Usa river wilayani Arumeru (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi)

TAARIFA YA CHADEMA KWA VYOMBO VYA HABARI KUTOKA SINGIDA

CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO –CHADEMA WILAYA (JIMBO) SINGIDA MJINI S.L.P 260, SINGIDA. 0784 – 462729 / 0767 – 462729 / 0754 – 818146 / 0754 – 487975 Tarehe 08/02/2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI JUU YA MASUALA NA KERO MBALI MBALI ZINAZOWAKABILI WANANCHI WA SINGIDA MJINI.

Chama cha DEMOKRASIA NA MAENDELEO – CHADEMA wilaya ya singida Mjini kimeanza kufanya mikutano ya ndani na hadhara kwenye kata zinazounda wilaya (jimbo) hilo kuanzia tarehe 07/02/2013 na mikutano hii kwa awamu ya kwanza itahitimishwa tarehe 15/02/2013.
 Leo tarehe 07/02/2013 Chadema kimefanya mkutano wa ndani katika kata ya Mtamaa ambapo mkutano huo ulifanyika pamoja na mambo mengine ulikuwa na lengo la kuibua kero zinazoikabili kata hiyo na kuangalia namna ya kuzitatua, kuandaa mkutano wa hadhara unaotarajia kufanyika wiki ijayo, kuimarisha chama kwenye ngazi ya msingi. Mkutano huo ulihutubiwa na viongozi wa wilaya akiwemo katibu mwenezi ndugu 1. MUTTA, Anselimi, 2. ANNA MGHWIRA kiongozi wa bawacha jimbo la Arumeru Mashariki, 3. NIWAEL MRUMA mratibu wa bawacha mkoa wa Singida,

 4. HAMISI MTIPA kamanda wa red briged mkoa wa Singida, Gideon mhasibu wa tawi la Chadema la uwanja wa ndege singida. Katika mkutano uliohudhuriwa na wanachama na wafuasi zaidi ya 30, palijitokeza masuala mbali mbali yakiwemo:

1. Kukatika kwa daraja linalounganisha barabara ya kutoka mjini hadi mtamaa, minyughe na viunga vyake. Nikishuhudia ubovu wa mawasiliano wa barabara hiyo kutokana na kukatika daraja hilo kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha mkoani singida,ni wazi wananchi wanapata taabu ya kufika na kutoka mjini hata gari letu lilikwama kupita pale na kulazimika kupitia kwenye korongo lililopo pembeni kitendo kilichopelekea gari kuzamisha magurudumu yake na kushindwa kutoka hadi tulipo pata msaada wa wananchi wasamalia wema. Sasa wananchi wanhoji kwanini mbunge tunashuhudia akigawa vitenge, kanga nk kupitia mabalozi na mkuu wa wilaya a viongozi wengine wanaotokana na CCM?

 2. Wananchi wanalalamika kuwa mikutano ya kiserikali inapoitishwa wananchi wengi hawapati taarifa mapema na wengine hawapati kabisa kitendo kinachopelekea wananchi washindwe kuwahoji viongozi wao ipasavyo juu ya masuala mbali mbali kwajili ya ujenzi wa kata na vijiji vyao. Hivyo wanatoa wito kwa viongozi wote wa serikali akiwemo diwani kuhakikisha wanatoa taarifa mapema juu ya mikutano hiyo ili wapate muda kujiandaa kuhudhuria mikutano hiyo.

3. Wanamlalamikia diwani wa kata ya mtamaa kuwa huwa hakusanyi maoni ya wananchi kabla hajaenda kuhudhuria vikao vya baraza la madiwani na hata anapokuwa ameenda huko na akirudi haleti mrejesho kwa wananchi wote. Hivyo wanamtaka ahakikishe anakusanya kero za wananchi waliomchagua bila kujali vyama vya siasa na itikadi nyingnezo.

4. Lakini wanahoji kauli ya rais Kikwete ya kusema kuwa wananchi kujipanga barabarani kusubiria magari yanayopita yakienda Mwanza au Dar es Salaam wawauzie mafuta yao ya zao lao la ALIZETI ndiyo masoko. Hivyo wananchi wanataka wawe na soko moja ambalo ni la kuaminika badala ya kusubiria magari ambayo hayaaminiki. Rais Kikwete alitoa kauli hiyo kwenye shere za kuapishwa kwa Dr. Alex Mkumbo kuwa askofu ambapo yeye (rais) alikuwa mgeni rasmi.

5. Lakini pia wanadai kuwa hawana mbunge bali wanamfadhili wa CCM na ndo maana anapogawa kanga anagawa zenye rangi ya CCM na anawapa wanaccm na sio wananchi wote. Ndiyo maana haonekani jimboni ili kutatua kero za wananchi akiwashirikisha juu ya utatuzi wa masuala mbali mbali na ndoiyo maana daraja limevunjika bila yeye hadi leo kutafuta ufumbuzi bali alichokiona kinafaa ni kugawa vitenge vyenye picha yake.

 MSIMAMO WA CHAMA JUU YA MASUALA HAYA 

1. Kutokana na hali ngumu ya mawasiliano iliyosababishwa na kukatika kwa daraja la mtamaa linalounganisha watu wa mtamaa na mjini litafutiwe ufumbuzi haraka iwezekanavyo kwani likiaachwa na kubaki hivyo lilivyo sasa hivi, litasababisha maafa makubwa ambayo yanaweza kugharimu maisha ya wananchi. Tunamtaka mkuu wa Wilaya kutumia mfuko wa maafa au kama ni mkurugenzi kuitisha kikao cha dharura cha baraza la madiwani kujadili ni jinsi gani ya kultafutia ufumbuzi daraja hilo na kama mvua itanyesha leo au kesho, kipande kilichosalia kinashilia kidaraja hicho kitaondoka.

2. Pia tunamtaka mkuregenzi kutoa hadharani gharama zilizotumika kujenga daraja hilo na kwanini livunjike mapema namna hii.

3. Tunamtaka mkaguzi wa ndani wa hesabu za serikali kufanya uchunguzi juu ya gharama halisi za mradi huo na ubora wa daraja hilo na ikiwa kutabainika kuna hujuma basi wahusika hata kama watakuwa wamehamishwa, wakamatwe na kuwekwa ndani na kulipa hasara ambayo imejitokeza kutokana na wananchi kukosa mawasiliano ya uhakika kutokana na kuharibika kwa daraja hilo. Ajabu ni pale ambapo ukifika hapo kuna basi lianalosimama ng’ambo ya upande mmoja ili wakifika hapo wafaulishwe kwenye gari linalosubiria upande wa pili na kuna vijana wanaokaa pale wakiwasaidia abiria kama ni mizigo na kudai kulipwa kidogo.

4. Tuna mtaka mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida kutuma makamanda wake kuchunguza utaratibu mzima uliotumika kumpata mkandarasi wa kujenga daraja hilo, kiasi cha fedha kilichotumika katika mradi huo na ubora/thamani ya daraja hilo, je, lilipokabidhiwa lilitakiwa kuishi kwa muda gani wa matumizi? Na ikibainika kulikuwa na ufisadi basi sheria ichukue mkondo wake ili kuthibiti vitendo vya kifisadi katika miradi inayojengwa kwa kodi za wananchi.

 5. Tunawataka viongozi wa kata na vijiji wa Kata ya Mtamaa akiwemo diwani kuhakikisha wanaitisha mikutano na kuwapa taarifa mbali mbali wananchi na mikutano hiyo ya vijiji na baraza la kata iwe ya wazi ili kutoa nafasi na fursa kwa wananchi kuhoji masuala mbali mbali kwa mstakabali wa maendeleo yao.

 6. Tunamtaka mbunge wa jimbo la Singida mjini kujitokeza hadharani na kuwaambia wananchi juu ya matumizi ya fedha za maendeleo ya mfuko wa jimbo toka ulipoanzishwa rasmi. Tunapata wasi wasi juu ya fedha wanazonunulia kanga na vitenge na kuwagawia wanaccm au kuandaa sherehe mbali mbali na kugawa fedha taslimu kama zile alizowahi kuwagawia walimu wa shule za msingi na sekondari Tzs 50,000/= kwa kila mwalimu zisijekuwa ndo hizo za mfuko wa jimbo. Haiwezekani wananchi wachangishwe michango ya elfu 20,000/= eti wanajenga maabara kwa amri ya rais ili hali haijulikani fedha za mfuko wa jimbo zimefanya nini.

7. Pia tunawataka madiwani wote wa kata zetu zote hususani kata za UTEMINI, NA MANDEWA kuwaeleza wananchi ni kwanini barabara za mitaani kwenye kata wanazoziongoza ni mbovu kupita kiasi? Ni hatua gani wanachukua kuhakikisha barua zinakuwa katika ubora unaotakiwa? Vinginevyo tutaandamana kudai haki za wananchi wetu. Haya ndiyo tunayoyataka kutafutiwa ufumbuzi na mambo mengine tutazidi kuyaweka wazi kwa kadri tunavyoendelea na mikutano yetu ambapo leo tutakuwa kwenye kata ya Unyamikumbi kijiji cha Ughaugha. Wito wangu kwa wananchi wa Singida (jimbo) mjini ni “ KUONDOA UOGA, NA KUDAI HAKI ZAO”

Imetolewa leo tarehe 08/02/2013 na: MUTTA, Anselimi (Mwl). Katibu mwenezi wa Wilaya ya Singida Mjini.

Kerry calls for action against Hezbollah

WASHINGTON, Feb. 6 (UPI) -- The United States is calling for international action against Hezbollah, which was tied to a Bulgarian bus attack, U.S. Secretary of State John Kerry said.

Bulgarian officials said Tuesday they had evidence to suggest Hezbollah was involved in the July bombing in Burgas, Bulgaria, that seemingly targeted Israeli tourists.

Hezbollah holds Cabinet-level positions in the Lebanese government but maintains a military wing that's waged war on Israel in the past.

Kerry, whose government considers the entire Shiite movement a terrorist organization, called on European allies to respond by cracking down on Hezbollah.

"We need to send an unequivocal message to this terrorist group that it can no longer engage in despicable actions with impunity," he said in a statement.

A spokesman for Catherine Ashton, Kerry's counterpart in the European Union, called for justice for those responsible for the July attack in Burgas.

"The implications of the investigation need to be assessed seriously as they relate to a terrorist attack on EU soil, which resulted in the killing and injury of innocent civilians" the statement read.

Hezbollah's terrorist designation isn't universal. Deputy Secretary-General Naim Qassem was quoted by The Daily Star newspaper in Lebanon as accusing Israel of "running a campaign of global terror against Hezbollah."

VICHWA VYA HABARI MAGAZETINI LEO IJUMAA 8/02/013










ASKOFU THOMAS LAIZER AFARIKI DUNIA, NI SIKU MOJA TU BAADA YA KUTEMBELEWA NA WAZIRI MKUU PINDA


Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisi ya Kaskazini.Askofu Thomas  Laizer amefariki duniaalasiri ya leo katika Hospitali ya Rufaa ya Selelian ya Mjini Arusha. Februari 6, 2013 Waziri Mkuu Mizengo Pinda,
alimtembelea  na kumjulia hali Askofu Thomas Laizer wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini Kati.
Taarifa zilipasha kuwa Askofu Laizer alilazwa Hospitalini hapo kwa zaidi ya mwezi mmoja, na hakuna daktari wala ndugu aliye tayari kusema ugonjwa unaomsibu.
Pinda alikwenda hospitalini hapo jana saa 9 alasiri na kukaa zaidi ya nusu saa, huku waandishi wa habari wakizuiwa kuingia katika chumba alimolazwa cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu.
Hata hivyo, baada ya kutoka katika chumba hicho kama ilivyo ada ya viongozi kuzungumzia hali ya mgonjwa, Pinda hakuzungumza na waandishi wa habari na kulikuwa na ulinzi mkali ambapo pia waandishi wa habari walizuiwa kuzungumza naye.