Saturday 23 February 2013

PICHA MBALIMBALI, WACHUNGAJI WA HUDUMA YA MAOMBEZI YA REDIO SAFINA WAKITOA MAOMBEZI SHEIKH AMRI ABEID LEO, KULIOMBEA TAIFA KUONDOKANA NA DHAMBI



DHAMBI iliyoachwa kwa muda mrefu bila kukemewa ni matokeo ya majanga yanayoikabili Tanzania hivi sasa na kusababisha mauaji ya watumishi wa dini ya Kikristo nchini, kufeli kwa wanafunzi kidato cha nne, mvua kutonyesha kwa wakati. 

Hayo yalielezwa jana jijini hapa na mchungaji Jovin Msuya wa huduma ya redio safina alipokuwa akihubiri kwenye kongamano maalum la kuiombea Taifa kuondokana na majanga hayo.

Mchungaji Msuya alisema matokeo ya dhambi hiyo ni vuguvugu la uvunjifu wa amani na utulivu ambao umejitokeza hivi sasa nchini na kwamba endapo waumini wa dini mbalimbali nchini hawatajitokeza kukemea matokeo yake ya baadae ni makubwa zaidi.

“Ili kutokomeza dhambi hizi ni wakati muafaka sasa kwa mamlaka za Kiserikali kwa kushirikiana na viongozi, taasisi na waumini wa dini zote nchini kutumia mamlaka walizokuwa nazo kukemea na kupatia suluhu vurugu ambazo zimekuwa zikitokea ili kurejesha amani na  utulivu ulioanza kutoweka,”alisema Msuya.

Aliwataka watanzania wa dini mbalimbali kuacha vurugu na uchochezi ndani ya nchi na badala yake kuhamasisha maombi ya kukemea roho za umauti  ambazo matokeo yake ni mauaji ya viongozi.

Alisema kila  jambo ambalo limekuwa likitokea nchini limekuwa na sababu yake kwa Mungu hivyo kuwataka watanzania kujiuliza sababu iliyopelekea kufeli kwa wanafunzi wahitimu wa kidato cha nne sanjari na mauaji ya  viongozi wa dini.

Aidha Mchungaji Christian Mwabukusi, alisema maovu mengi ambayo yamekuwa yakitokea ndani ya jamii yamekuwa yakichangiwa na ugumu wa maisha waliyokuwa nayo watanzania kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa ajira.

Alisema maombezi kwa Taifa yanayofanywa na redio hiyo yatakuwa yakifanyika mara moja kila baada ya miezi mitatu na kutoa wito kwa watanzania kuungana katika maombi hayo ili kunusuru Taifa katika dhambi.


WAUMINI WAKIWA WAMENYANYUA MIKONO JUU KULIOMBEA TAIFA

WAUMINI WA KIKRISTO JIJINI ARUSHA WAKIANDIKA MISTARI YA BIBLIA ILIYOKUWA IKITAJWA NA WACHUNGAJI



WACHUNGAJI WA MADHEHEBU MBALIMBALI YA KIKRISTO NCHINI WAKIWA WAMENYANYA MIKONO KUSHIRIKI MAOMBI YA KULIOMBEA TAIFA KUONDOKANA NA DHAMBI, WA KWANZA KULIA NI MCHUNGAJI ANDREW KAJEMBE WA KANISA LA ST.JAMES ARUSHA

WAUMINI WA MADHEHEBU MBALMBALI YA KIKRISTO JIJINI ARUSHA WAKIWA WAMEJIFUNIKA KWA MIAVULI NA KANGA KUZUIA JUA KALI LILILOKUWA LIKIWAKA UWANJANI HAPO

MCHUNGAJI WA HUDUMA YA MAOMBEZI NA REDIO SAFINA JOVIN MSUYA AKITOA MAHUBIRI

MCHUNGAJI CHRISTINE MWABUKUSI AKITOA MAHUBIRI KATIKA KONGAMANO HILO


WAKIWA WAMENYANYUA MIKONO JUU WAKIIMBA NYIMBO ZA MAPAMBIO KUOMBEA NCHI YETU

WAUMINI WAKISIKILIZA MAHUBIRI

No comments:

Post a Comment