Monday 4 February 2013

TASWIRA ZAIDI HAPPY BIRTHDAY YA CCM

Vijana wa Chipukizi wakiimba wimbo wa Kwaya katika maadhimisho hayo

Vijana wa Chipukizi wa CCM wakipita kwa Gwaride la Heshima na Utii mbele ya Rais Jakaya Kikwete.

Wananchi wakiwa wamefurika kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdurahman Kinana akizungumza katika maadhimisho hayo.

Kikundi cha ngoma kutoka nchini Burundi kikitumuiza katika maadhimisho hayo yaliyofanyika leo kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza katika maadhimisho hayo katika uwanja wa Lake Taganyika.

Msanii Diamond akiongoza kundi lake katika kutoa burudani kwa wananchi waliojitokeza katika maadhimisho hayo.

Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe akizungumzia mikakati ya Serikali katika maadhimisho hayo juu ya urejeshaji wa huduma za treni katika kituo cha Reli ya Kati cha Kigoma.

Rais Jakaya Kikwete akiangalia picha zilizochorwa zikimuonesha yeye na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius K. Nyerere wakati alipotembelea mabanda ya maonyesho katika maadhimisho ya miaka 36 ya CCM

Rais Jakaya Kikwete akiangalia ndizi zinazozalishwa mkoani Kigoma katika banda la wakulima wa ndizi kutoka mkoa huo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dk. Jakaya Kikwete akihutubia wananchi katika sherehe za miaka 36 ya CCM zilizofanyika jioni ya leo kwenye uwanja wa Lake Tanganyika Mkoani Kigoma na kuhudhuriwa  na wananchi mbalimbali waliojitokeza kushiriki katika sherehe hizo.


Rais Jakaya Kikwete akiwapungia mkono wananchi wa mkoa wa Kigoma waliojitokeza kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya CCM kwenye uwanja wa Lake Tanganyika

Wananchi mbalimbali wakiwa wamejitokeza kwenye uwanja wa Lake Tanganyika.

Katibu wa Halmashauri kuu ya CCM Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimtunza mmoja wa wasanii wadogo wa kikundi cha ngoma kutoka nchini Burundi kilichoshiriki katika maadhimisho ya miaka 36 ya CCM.
PICHA KWA HISANI YA  mjengwablog

No comments:

Post a Comment