Monday 7 January 2013

Mwanafunzi wa kike Brazil anadi bikira yake ili aweze kugharamia tiba ya mama yake aliyepooza.



Binti Rebbeca Bernardo akiwa nyumbani kwao akimuuguza mama yake aliyepooza mwili.

Binti Rebecca Bernardo.
Mwanafunzi mmoja wa sekondari mkazi wa mji wa Sapeacu nchini Brazil Rebbeca Bernardo (18) amefikia uamuzi wa kuinadi bikira yake katika mtandao ili kupata fedha za kugharamia matibabu ya mama yake aliyepooza mwili.
Rebecca amedai kuwa alijaribu kufanya kazi za kuuza vipodozi na pia kufanya kazi ya uhudumu lakini kazi zote hizo hazikumpatia kipato cha kumwezesha kumudu gharama za kumtunza mama yake.
Mwanafunzi huyo amesema amefikia uamuzi huo baada ya kuvutiwa na jinsi mwanamke mwingine aliyejulikana kwa jina la Catarina Migliorini mwenye umri wa miaka 20 ambaye mwishoni mwa mwaka jana aliweza kupata kiasi cha dola 780,000 kwa kuiuza bikira yake kwenye mnada.

Rebecca amedai kuwa Catarina alipata wadau mbalimbali kutoka kona zote za dunia ambao walitaka kuivunja bikira yake na yeye pia anatarajia wanaume wengi watajitokeza.
Katika mchakato wake huo wa kuinadi bikira yake, Rebecca amedai kuwa jumla ya wanaume watatu wameshajitokeza na dau kubwa hadi sasa ni dola 35,000.

No comments:

Post a Comment