Monday 7 January 2013

PICHA MBALIMBALI RAIS JK ALIPOHUDHURIA MISA YA KUSIMIKWA KWA ASKOFU WA DAYOSISI YA KANDA YA KATI SINGIDA DKT ALEX MKUMBO

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Askofu Mteule jimbo la Singida, Dkt Mkumbo muda mfupi baada ya kusimikwa

RAIS KIKWETE KATIKATI AKIWA NA ASKOFU MKUU WA KKKT KULIA PAMOJA NA ASKOFU MTEULE WA DAYOSISI YA KATI DKT MKUMBO WA KWANZA KULIA

Rais  Jakaya Kikwete (wa tatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Askofu mteule wa KKKT dayosisi ya kati, Dk.Alex Mkumbo na msaidizi wake Cprian Yohana Hilinti (wa pili kulia).Akina mama hao ni wake wa askofu Dk.Mkumbo na msaidizi Hilinti. (Picha na Nathaniel Limu).

RAIS JAKAYA KIKWETE AKISALIMIANA NA ASKOFU MKUU WA KKKT ALEX MALASUSA MJINI SINGIDA JANA

RAIS KIKWETE KATIKA KIKAO CHA NDANI NA VIONGOZI WA MKOA WA TABORA

RAIS KIKWETE AKIKAGUA TAARIFA ZA MAENDELEO YA MKOA WA TABORA FATMA MWASA, RAIS KIKWETE YUKO MKOANI TABORA KWA ZIARA YA KIKAZI

RAIS KIKWETE KATIKA PICHA YA PAMOJA NA MAASKOFU WA KKKT PAMOJA NA MKUU WA MKOA WA SINGIDA PARSEKO KONE ALIYEVAA TAI NYEKUNDU PEMBENI MWA ASKOFU MKUU KKKT ALEX MALASUSA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dk.Jakaya Mrisho Kikwete,ameyahimiza madhehebu mbalimbali ya dini nchini, kufufua utaratibu uliokuwepo zamani wa kufanya vikao  baina yao, ambavyo pamoja na mambo mengine,vilisaidia kuimarisha mahusiano mazuri na kuheshimiana.
Dk.Kikwete ametoa wito huo jana (6/1/2013) wakati akizungumza kwenye sherehe za kusimikwa kwa askofu mteule wa Kanisa la kiinjili la kilutheri dayosisi ya kati,Dk.Alex Seif Mkumbo, kuongoza kanisa hilo kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.  Alisema utaratibu huo uliepusha vitendo vya kukashifiana, kudharaulina na kutokuvumiliana.
Alisema hivi sasa vitendo vya kudharauliana,kuchochea vurugu na chuki baina ya madhehebu ya dini,vimechangiwa kwa kiasi kikubwa na kuachwa kwa utaratibu huo ambao ulisaidia mno kudumisha amani na utulivu.
“Hivi sasa watu wanasema sana, wala hawaogopi kusema,mambo sasa hivi ni tofauti mno.Wapo watu wanakipaji cha kuchochea chuki na kuchochea kudharauliana kwa  dhehebu moja na jingine.Bila vikao vya madhdhebu ya dini,watu hawa watasababisha hata uhuru wa kuabudu kutoweka”,alisema na kuongeza; “Utaratibu huu wa kukutana madhehebu kwa madhehebu,utaepusha taifa letu na machafuko  ya kidini”.
Dk.Kikwete alisema kutokana na ukweli huo,upo umuhimu kwa madhehebu ya dini kufufua/kuhuisha utaratibu wa kufanya vikao baina ya madhehebu  ili amani,utulivu,kuheshimiana na kuvumiliana kuweze kudumu.
Aidha,ametumia  fursa hiyo kuwahimiza viongozi wa madhehebu  kutekeleza majukumu yao bila kuchoka ikiwemo kuhimiza uadilifu na kukemea vitendo vyote viovu katika jamii.
Awali askofu mkuu wa KKKT nchni.Dk.Alex Mwalasusa, alimwahidi rais Kikwete kuwa wataendelea kushirikiana na serikali katika kuwaendeleza Watanzania kiroho na kimwili.

No comments:

Post a Comment