Sunday 28 October 2012

CHADEMA MOTO ARUSHA, YAIGARAGAZA CCM MAENEO MENGINE

Umati wa wafuasi wa Chadema wakisikiliza viongozi mbalimbali siku ya mwisho ya ufungaji wa kampeni katika kata ya daraja mbili. katika uchaguzi huo uliomalizika jana, diwani wa Chadema aliibuka mshindi kwa kura nyingi.
Na mwandishi wetu

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kuonyesha imani yake kubwa kwa watanzania baada ya jana mgombea wake kuibuka mshindi katika kata ya Daraja mbili.

uchaguzi huo wa Daraja mbili ulikuwa unarudiwa baada ya diwani wake wa awali kwa tiketi ya (CCM) Bashir Msangi kufariki dunia ghafla mapema mwaka huu.

Matokeo katika Kata hiyo ya Daraja Mbili, yalionyesha CHADEMA ineweza kujikusanyia kura 2192 dhidi ya 1315 za mgombea wa chama tawala.

Hata hivyo uchaguzi huo ambao ulifanyika kwenye kata 29 katika halmashauri mbalimbali nchini, umemalizika huku vurugu kubwa zikitawala na kusababisha wafuasi wa vyama hivyo kuumizana.

Hadi sasa matokeo ya kata 14 yanaonyesha kuwa CCM ilikuwa imefanikiwa kurejesha kata zake saba, huku CHADEMA ikinyakua kata sita, ambapo mbili zilikuwa za kwao na nne imewanyang’anya CCM na CUF ikiwa na kata moja.


matokeo ya udiwani katika baadhi ya kata yalikuwa yakiendelea kutolewa huku CHADEMA ikiendelea kuikaba CCM kwa kuzitwaa baadhi ya zilizokuwa kata zake.

CHADEMA wameweza kuzirejesha kata zao mbili za Nangerea jimboni Rombo, ambapo mgombea wao Frank Sarakana alijizolea kura 2370 dhidi ya 1134 za Dysmas Silayo wa CCM pamoja na ile ya Mtibwa, mkoani Morogoro.


Wilayani Sikonge katika kata ya Ipole, CCM walipoteza kata hiyo kwa CHADEMA iliyopata kura 577 dhidi ya 372 za washindani wao, na vilevile kuitwaa kata nyingine ya Lengali wilayani Ludewa iliyokuwa ya CCM.


CHADEMA pia ilikuwa ikiongoza katika kata ya Mpwapwa, mkoani Dodoma, hadi tunakwenda mitamboni usiku.


Nayo CCM ilifurukuta kwa kuzirejesha kata zake za Msalato ya mkoani Dodoma, Bang’ata ya Arumeru Magharibi kwa kuwa 1177 dhidi ya 881 za CHADEMA, Mletele ya Songea CCM ilishinda kwa kura 950 na CHADEMA ilipata 295.


Pia CCM iliweza kutetea kata zake za Mwawaza mjini Shinyanga, Lwenzela mkoani Geita, Bungala wialayni Kahama na Bagamoyo mkoani Pwani kwa kuibwaga CHADEMA wakati Chama cha Wananchi (CUF) kilishinda kata ya Newala.

No comments:

Post a Comment