Friday 26 October 2012

HABARI YA KUSIKITISHA JANA




Kupigwa kwa bomu nyumbani kwa Katibu wa Bakwata Mkoa wa Arusha Abdul Kareem Jonjo. Baadhi ya vongozi wa ulinzi na usalama Mkoa wa Arusha wakiongozwa na mkuu wa Mkoa wa Arusha wakiwa kwenye matukio mbali mbali nyumbani na hospitalini jijini hapa leo baada ya tukio la kupigwa kwa bomu kwa katibu huyo nyumbani kwake eneo la Mtaa wa Kanisani Kata ya Sokon 1 jijini hapa.
  



Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo akimjulia hali Katibu Mkuu wa Bakwata Mkoa wa Arusha Abdulkareem Jonjo jana katika hospitali ya Mt. Meru.  vongozi mbalimbali wa ulinzi na usalama Mkoa wa Arusha walimtembelea katibu huyo hospitalini Mt.Meru kumjulia hali. tukio la kupigwa kwa bomu kwa katibu huyo lilitokea usiku wa jana nyumbani kwake eneo la Mtaa wa Kanisani Kata ya Sokon 1 jijini hapa.

No comments:

Post a Comment