Friday 23 November 2012

KESI INAYOMKABILI LEMA SASA DESEMBA 4, MWAKA HUU



KESI INAYOMKABILI LEMA SASA DESEMBA 4, MWAKA HUU

Kesi Uchaguzi inayomkabili aliyekuwa mbunge wa jimbo la Arusha mjini Godbless Lema wa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo{CHADEMA} itasikilizwa desemba 4  mwaka huu katika mahakama ya rufaa Jijini Dar es salaamu.

Awali mahakama ya rufaa yenye majaji watatu wakiongozwa na Jaji Mkuu Othmani Chande novemba 8 mwaka huu iliamuru mkata rufaa Leman a wakili wake Method Kimomogolo kurekebisha rufaa yao iliyokuwa na makosa mengi ya kisheria ndani ya siku 14.

Chande akiwa na majaji wengine Salumu Masati na Nathalie Kimaro walimtaka lema kuwalipa mawakili wawili Alute Mungway na Modesti Akida gharama zao za kuja Jijini Dar es salaamu kuja kusikiliza kesi hiyo .

Kwa mujibu wa hukumu hiyo ya pingamizi iliyotolewa siku hiyo pia Mbunge huyo wa zamani ametakiwa pia kuwalipa gharama zote wanachama watatu wa Chama Cha Mapinduzi[CCM} waliofungua kesi hiyo kwa kwenda Jijini Dar es salaamu.


Akizungumza na gazeti hili jana Mussa Mkanga alisema kuwa tayari amepewa hati ya kuitwa katika mahakama ya rufaa siku hiyo na wao wameshaanda gharama ya kesi hiyo kama walivyoamuriwa na Mahakama hiyo lakini hakuwa tayari kutaja kiasi cha gharama hiyo kwa madai kuwa mpaka itakapowasilishwa katika mahakama hiyo.


‘’Nafikiri wamesharekebisha rufaa yao kwani walipewa muda wa siku 14 kuirekebisha na muda umeshapita na sisi tumeshapewa hati ya kuitwa katika mahakama hiyo kusikiliza kesi hiyo na tayari tumeshakamilisha mahesabu yetu ya gharama zetu’’ alisema Mkanga


Wakati huo huo Mkanga pia alizungumzia uvumi ulioenea Jijini Arusha hususani katika mitandao ya kijamii kuwa amepooza mwili mzima baada ya kuendelea kufuatilia sana kesi hiyo na kueleza kuwa maneno hayo sio ya kweli kwani yeye ni mzima wa afya na hana ugonjwa wowote hata ‘’homa ya mafua’’.

Alisema wale wote wenye nia mbaya ya kumwombea yeye kupata ugonjwa huo iko siku mungu atawalipiza wao kwani siku zote mungu hapendi mcha mungu kumwombea mwenzake mabaya.

No comments:

Post a Comment