Friday 23 November 2012

WANAFUNZI WAPANGIWA UTARATIBU WA KUCHANGIA JAMII



WANAFUNZI WAPANGIWA UTARATIBU WA KUCHANGIA JAMII 

WANAFUNZI wa kidato cha nne,tano na sita katika shule binafsi ya Mtakatifu Costantine ya jijini Arusha wamepangiwa utaratibu na uongozi wa shule hiyo wa  kuchangia jamii inayowazunguka kabla ya kupata cheti cha kuhitimu elimu yao.

Katika kuitia wito huo wanafunzi wanne wa shule hiyo wa kidatu cha sita Novemba 16 mwaka huu wamechanga jumla ya shilingi milioni 4,155,000 ambazo zitawasaidia wanafunzi wa nyumba tatu za watoto yatima ambao wako sekondari wa Jijini Arusha

Wanafunzi waliojitoa na kuamua kuonyesha njia na kuitikia wito wa uongozi wa shule ni pamoja na Aljawaad Hassanali,Kush Lodhia ,Nuzhat Hatema na Shilia Patalia.

Akizungumza mara baada ya kukusanywa kwa fedha hizo taslimu ,Hassanali alisema mbali ya kusaidia nyumba tatu za watoto yatima pia fedha hizo zitapelekwa kwa wanafunzi 6 wa sekondari wenye mtindo wa akili (kwenye shule maalumu za walemavu).

Alisema kuna wanafunzi 90 wa kidatu cha nne, tano na sita katika shule ya Constantino na wote wametakiwa kusaidia jamii vinginevyo huruhusiwi kupata cheti cha kumaliza shule mpaka utimize lengo hilo ambalo sisi wanafunzi tunakumbushwa kusaidia jamii isiyi jiweza ambayo inayotuzunguka.

‘’hatuna shida na kuchangia hilo kwani ni jukumu la kina mwanadamu na uongozi wa shule ulipoamua na kupitisha hilo hakuna mzazi wala mwanafunzi aliyebisha na kinachotakiwa ni kujipanga na kuangalia wapi kwa kusaidia ‘’alisema

Mmoja wa wazazi wa mtoto anayesoma katika shule hiyo ambaye aliombakutotajwa jina alisema kuwa mpango huo unawajenga wanafunzi kuwa na ukarimu kwa jamii wakiwa wadogo na hiyo itasaidia sana wanafunzi hao.

Alisema uongozi wa shule umebuni mkakati mzuri sana kwa wanafunzi wanasoma katika shule hiyo wa vidatu hivyo kuwa na ukarimu kwa jamii kwa kusaidia watoto wengine hususani wenye uwezo mdogo,walemavu na yatima.


No comments:

Post a Comment